Unaweza kusema mlinda lango Moussa Camara leo alikuwa na siku mbaya kwani aliruhusu mabao mawili yanayofanana yote yakifungwa kutokea nje ya 18
Simba ilitangulia kufunga mabao yake mawili katika kipindi cha kwanza kupitia kwa Mohammed Hussein na Lionel Ateba aliyefunga kupitia mkwaju wa penati
Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema hayakuwa matokeo mazuri kwao kwani walikuwa na nafasi ya kushinda mchezo huo
"Tunacheza vizuri na kutengeneza nafasi nyingi lakini tunapaswa kuongeza ukatili mbele ya lango. Wapinzani wetu wamepata nafasi mbili na wamefunga mabao mawili, sisi tulipata nafasi nyingi zaidi hatukuzitumia ipasavyo"
0 Comments